Siasa
Wizara ya Katiba yaomba Bil. 272 bajeti ya 2022/2023
Wizara ya Katiba na Sheria imeomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi bilioni 272.7 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2022/2023.
Kati ya Fedha hizo, Shilingi bilioni 207.7 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Shilingi 65 ni kwa ajili ya matumizi ya miradi ya maendeleo.