Young Dee akirekebisha makosa aliyofanya Mtu Chee ruksa kurudi kundini – Stamina
Kwa mujibu wa Stamina kuondoka kwa Young Dee kwenye kundi la Mtu Chee kulitokana na kupishana kauli kati yake na Country Boy, na kwamba kama atarekebisha makosa aliyowafanyia wako radhi kumrejesha kundini.
Hivi karibuni Young Dee alithibitisha tetesi za kutumia madawa ya kulevya na kutangaza kuwa ameacha. Wiki hii ameachia ngoma yake mpya ‘Hands Up.’
“Kulikuwa na misunderstanding baina yake yeye na Country Boy,” Stamina alimweleza mtangazaji wa Jembe FM, JJ.
“Anytime kama ataona yeye ndio alikosea kama alivyorekebisha mistakes zake katika management yake, kama ataweza kurekebisha mistakes zake pia kwenye kundi anakaribishwa anytime hakuna mtu mwenye bifu naye ni mambo tu ya kikazi na kipindi cha kati alipokuwa amechanganyikiwa na madude yake hayo kwahiyo ndio maana ilikuwa ni ngumu kuweka kukaa chini na kusolve chochote,” aliongeza.
“Lakini sasa hivi kama yupo competent kabisa anaona anaweza kusolve chochote anakaribishwa muda wote.”
Miezi kadhaa iliyopita Mtu Chee waliachia ngoma bila Young Dee na kumshirikisha Young Killer.