Tragedy
Kwa Heri Shekh Yahaya Hussein
Mnajimu wa Afrika mashariki na kati Shekh Yahaya Hussein (89) inayekadiliwa kuwa na watoto 20, amefariki dunia jana saa 4; 30 asubuhi katika hospitali ya Mount Ukombozi kwa maradhi ya moyo.
Mwanaye Hassan Yahaya Hussein amethibitisha kifo hicho, na kusema baba yake alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa huo kwa muda mrefu, na hata raisi Jakaya Mrisho Kikwete aliwahi kumpeleka nje ya nchi kwa matatibabu.
Pia alisema mazishi yanategemewa kufanyika leo Mei 21, katika makabuli ya Tambaza.
Mungu ailaze roho ya marehemu, mahari pema peponi.
AMIN…………
Marehemu Shekh Yahaya Hussrin ezi ya Uhai wake.