Burudani

Nay wa Mitego apokea vitisho kutoka kwa watu aliowatuhumu kuchukua pesa za msiba wa Ngwea

Msanii wa Hip Hop, Nay Wa Mitego amesema haogopi vitisho anavyoendelea kupata baada ya watu aliowatuhumu kwenye wimbo wa mpya, Salam Zao’ kuwa walichukua pesa za rambirambi za msiba wa marehemu Albert Mangwair.

1173664_401068240004866_1674635065_n

Kupitia akaunti zake za Facebook na Instagram, Nay ameanza kuandika na kufichua vitisho anavyopokea na huku akiwataka waliochukua pesa za marehemu Ngwair wazirudishe kimya kimya.

“Zipo nyingi zingine za vitisho,nitazipost zote watu wangu mujue leo nimeanza na iyo..!! Ukweli unauma sana!! siogopi vitisho vyenu,, pelekeni hela kwa ndugu wa marehem bado nafasi mnayo ata kimya kimya,, mi Nikifa sihitaji kamati za ki**enge kwenye msiba wangu, maana watu wanafanya misiba yetu mitaji yao,” ameandika Nay.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents