Burudani

Willow Smith aachia albamu yake ya pili kwenye birthday yake

Msanii Willow Smith ambaye ni mtoto wa waigizaji maarufu duniani Will na Jada Smith, ameachia albamu yake ya pili katika siku yake ya kuzaliwa.

Willow ambaye Jumanne hii ametimiza miaka 17 ameachia albam yake hiyo iitwayo ‘The 1st’ ambayo ina ngoma 11 ndani yake.

Awali msanii huyo ambaye yupo chini ya lebo ya Roc Nation ya Jay Z aliachia albam yake iitwayo ARDIPITHECUS ambayo ilikuwa ni Disemba 11 ya mwaka 2015. Hizi ni nyimbo ambazo zinapatikana katika albamu yake hiyo mpya.

1.Boy
2.An Awkward Life of an Awkward Girl
3.And Contentment
4.Ho’ ihi Interlude
5.Israel
6.Oh No!!!
7.Warm Honey
8.Human Leech
9.Lonely Road
10.A Reason
11.Romance

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents