Burudani

Majanga mapya yamkuta Soulja Boy akijiandaa na pambano lake na Chris Brown

Wakati akijiandaa na pambano lake la ngumi dhidi ya Chris Brown, majanga yameanza kumkuta rapper Soulja Boy.

Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, Jumanne hii nyumba ya rapper huyo iliyopo Hollywood Hills ilivamiwa na mwizi aliyefanikiwa kuondoka na fedha kiasi cha $10,000 pamoja na vitu vyenye thamani ya $12,000.

Hata hivyo imedaiwa kuwa kamera zilizofungwa katika eneo hilo zimefanikiwa kupata picha ya mwizi huyo ambapo polisi wanaendelea kumfuatilia. Japo kumekuwa na mvutano juu ya pambano lake na Chris Brown lakini hakuna ushahidi wowote unaonyesha kuwa wizi huo umefanywa na watu wa upande wa Chris kama kumchanganya Soulja Boy.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents