Michezo
Chelsea kumsajili Lukaku na Barkley kwa paundi 100m
Klabu ya Chelsea inataka kufanya usajili wa wachezaji mawili wa Everton Ross Barkley na Romelu Lukaku, kwa mujibu wa mtandao wa Telegraph.
Ripoti zinadai kuwa Lukaku anatamani kurejea Chelsea wakati Barkley ni mchezaji ambaye alikuwa akitakiwa siku nyingi na Chelsea.
Chelsea inajipanga kwa pamoja kutoa kitita cha paundi milioni 100 ikiwa itaweza kuishawishi Everton kuuza nyota hao wawili.