Burudani

Kesi ya Rob Kardashin na Blac Chyna yapata muafaka

Rob Kardashian na Blac Chyna ambao sasa ni kama paka na chui, walifikisha mahakani siku ya jana ambapo Rob alifunguliwa mashtaka ya udhalilishaji juu ya mpenzi wake huyo.

Katika kesi hiyo Rob amewekewa vizuizi vya kutomsogelea mzazi mwezake wala kumtolea maneno machafu na yakashfa.

Pia inadaiwa wawili hao wamewekeana makubaliano yasio ya kimaandishi juu ya haki ya kila mtu katika kumlea mtoto wao Dream mwenye miezi nane, ambapo Rob atakuwa naye kwa muda wa siku nne, huku siku zingine atakua kwa mama yake.

Chanzo cha karibu kimeeleza kuwa Rob na Blac Chyna hawana mpango wa kufikishana mahakamani tena juu ya kupena haki za kumlea mtoto kwani wameshakubaliana ila wanafanya utaratibu wa kuweka makubaliano hayo katika maandishi.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents