Burudani
Aliyemchapa kofi Justin Timberlake akamatwa
Mtu mmoja ambaye anadaiwa kumzaba kofi msanii Justin Timberlake katika mchuano wa gofu katika Ziwa Tahoe huko Nevada amekamatwa.
Katika video iliopatikana na mtandao wa TMZ,Justin anaonekana kupita katikati ya watu kabla ya mkono wa mtu kuonekana ukimgusa upande mmoja wa uso wake.
Hii ndo video yenyewe
https://youtu.be/Bq_nn0aiQU0
Justin aligeuka na kumuuliza, ndugu mbona unafanya kitendo kama hicho?
Walinzi wake walimvuta msanii huyo mwenye umri wa miaka 35 lakini baadaye akaonekana akizungumza na mshukiwa huyo.