Burudani

Barakah The Prince: Uhasama wa Alikiba na Diamond ulikuwa na athari kwenye Nisamehe

Barakah The Prince amedai kuwa kumshirikisha Alikiba kwenye wimbo wake Nisamehe kulikuwa na changamoto hasa kutokana na mvutano uliopo kati ya Team Kiba na Team Diamond.

“Ujue Alikiba ni brand kubwa na ni brand ambayo ina mvutano na vitu vingi, kwahiyo unavyofavya collabo na Alikiba kuna mawili hapo, kuna nyimbo kufanya vizuri na kuna nyimbo kufanya vizuri wastani, wa kawaida kwasababu ya ule mvutano wa kibiashara ambao upo kati yake na timu nyingine,” Barakah alikiambia kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz cha Salama Jabir.

Hata hivyo amesema hakutegemea kama wimbo huo ungekuja kufanya vizuri kama ngoma zake zingine.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents