Burudani

Ben Pol: Nafikiria kufanya collabo na Jason Derulo

Mfalme wa R&B Tanzania, Benard Michael Paul a.k.a Ben Pol ameweka wazi mipango yake ya kuupeleka muziki wake kimataifa kwa kutafuta collabo na wasanii wakubwa wa kimataifa.

ben pol Kenya

Ben Pol ambaye kwa sasa yuko nchini Kenya alikoenda kushiriki kwenye msimu mpya wa kipindi cha Coke Studio Africa, amesema kuwa miongoni mwa wasanii ambao anategemea kufanya nao collabo ni pamoja na hit maker wa “Wiggle”, Jason Derulo kutoka Marekani.

Hit maker wa “Sophia” ameweka wazi mpango huo alipokuwa katika session ya kuulizwa maswali na mashabiki kupitia ukurasa wa Facebook wa Coca Cola.

Shabiki alimuuliza Ben pol endapo akipata nafasi ya kuchangua msanii wa kufanya naye collabo wa kimataifa atamchagua nani?

“Kwa sasa nafikiria kufanya collabo na Jason Derulo, kwa sababu ni msanii mchapakazi na anayezidi kukua na kuvuka mipaka siku hadi siku, Menejimenti yangu inaendelea kumtafuta, natumai tutafanikiwa.” alijibu Ben Pol.

Hadi sasa Ben Pol tayari amefanya collabo na Nameless na Rabbit wa Kenya.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents