Burudani
Billnass azungumzia tuhuma ya kuwa TID anatumia madawa ya kulevya
Msanii wa muziki kutoka ‘label’ ya Radar Entertainment, Billnass amesema kuwa hajawahi kumuona TID akitumia Madawa ya Kulevya kama maneno yanavyoongelewa mitaani.
Akizungumza katika kipindi cha The Playlist cha Times Fm Jumamosi hii, rapa huyo ameshangazwa na maneno hayo ambayo amedai hajui yanatokea wapi.
“Sijui haya maneno yanatokea watu, ni vitu ambavyo watu wanatumia kwa siri sana ila mimi sijawahi kumuona TID akitumia, na tunasafiri kila kwenda sehemu kibao hata dalili za mtu anayetumia madawa ya kulevya sijawahi kuziona kwa TID. Sijui sijawahi kumuona kwa kweli”, alisema
Billnass kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya uitwao ‘Chafu Pozi’.