Burudani

Davido aingia studio na Tinashe na Rae Sremmurd

Tangu asaini record deal na Sony Music, staa wa Nigeria, Davido amekuwa akijichanganya na mastaa wanaohit Marekani.

13183284_1715266045380170_859897737_n

Hivi karibuni alishare picha kwenye Instagram akiwa na muimbaji mrembo, Tinashe, kitu kinachoonesha wazi kuwa wanatengeneza ngoma ya pamoja.

13129354_275301092807428_616799848_n

“How long will you wait … @tinashenow,” aliandika Davido kwenye picha moja akiwa na muimbaji huyo ambaye jina lake halisi ni Tinashe Jorgenson Kachingwe na mwenye asili ya Zimbabwe.
“Can u make me feel like number 1 ??? @tinashenow,” aliandika kwenye picha nyingine.

Tinashe amehit sana Marekani na nyimbo zake kama 2 On, All Hands on Deck na Player aliyomshirikisha Chris Brown.

13117806_1080228078716269_504997542_n

Pia Davido alishare picha akiwa na rappers ndugu, Khalif “Swae Lee” Brown na Aaquil “Slim Jimmi” Brown wanaounda kundi la Rae Sremmurd.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents