Burudani
EFM kujenga madarasa ya shule za sekondari Kinondoni
Kituo cha redio cha EFM cha jijini Dar es Salaam, kimekabidhiwa michoro ya ramani ya madarasa ya sekondari wilaya ya Kinondoni kata ya Kimara kwaajili ya kuanza kuyajenga kama ilivyoahidi.
Mkurugenzi Mkuu wa Efm Radio, Francis Siza akipokea ramani ya michoro ya madarasa kutoka kwa Afisa elimu wa wilaya ya Kinondoni Bwana Rogers J. Shemwelekwa
Makabidhiano yaliyofanyika katika ofisi za Kituo hicho cha Utangazaji kupitia masafa ya 93.7 Jumatatu hii.
Afisa elimu wa wilaya ya Kinondoni Rogers J. Shemwelekwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Efm baada ya makabidhiano ya michoro ya madarasa.Kushoto ni Mkurungezi mkuu wa Efm Radio Fransis Siza, (kulia) ni Mhariri Mkuu Scholastica Mazula na meneja mahusiano na mawasiliano Denis Ssebo