Michezo
Farhan Kihamu awapiga dongo Simba
Mchambuzi wa Clouds Media Farhan Kihamu kwenye mtandao wake wa X amesema “Yanga jana kafungwa ghafla tu ule mjadala wa GSM kudhamini time nyingi umeisha, ndipo hapo utakuja kugundua shida haikuwa udhamini, shida ilikuwa ni propaganda kutokana na FORM ya Yanga.”
“Angefungwa Azam ghafla tu ule mjadala wa Dube ungeshika kasi, wangekazia suala la Viongozi wa Azam kura Mashabiki wa hizi timi za Kariakoo, huenda wale wenye mlengo wa Yanga wangekuwa matatizoni.” anasema Farhan.
Aliendelea na kusema “Yanga ikianza tena kushinda mfululizo utaibuka mjadala mwingine, huenda ukaja wa kwanini Viongozi wao wanaenda uwanjani kila mechi, Tanzania hii hakishindikani kitu.”
Imeandikwa na Mbanga B.