Burudani
Filamu ya Noah yazuiliwa kuoneshwa nchini China
Mamlaka za nchini China zimegoma kuruhusu kuzinduliwa kwa filamu ya Noah iliyochezwa na Russell Crowe, ambayo tayari imepigwa marufuku katika nchi za kiislamu.
Filamu hiyo imekatwa kuoneshwa katika nchi za Bahrain, Indonesia, Malaysia, Qatar na kwingine. Hata hivyo inasemekana kuwa kukatazwa kuzinduliwa kwa filamu hiyo nchini China ni kwasababu za kibiashara kwakuwa filamu zingine kama Godzilla zitazinduliwa hivi karibuni.