Herve Renald atangaza rasmi kikosi cha Morroco kitakachoivaa Cape Verde
Kocha mpya wa Morocco ambaye pia ni raia wa Ufaransa, Herve Renald ametangaza rasmi kikosi chake kitakachoivaa Cape Verde kwenye kusaka tiketi ya kushiriki michuano ya AFCON 2017.
Herve Renald amefanikiwa kuchukua kombe la AFCON akiwa na timu mbili tofauti, Zambia mwaka 2012 na Ivory Coast mwaka 2015. Kocha huyo amechukua mikoba ya Badou Zaki ambaye alikuwa akiifundisha timu hiyo ya Morocco.
Kikosi alichokitangaza Renald ni makipa, Mounir El Kajoui (Numancia), Yassine Bounou (Real Zaragoza), Abdelali M’Hamdi (RSB Berkane).
Walinzi, Mehdi Benatia (Bayern Munich), El Kaoutari (Reims), Issam Chebake (Le Havre), Achraf Hakimi (Real Madrid B), Nabil Dirar (Monaco), Marouane Da Costa (Olympiakos), Mohamed Oulhaj (Raja Casablanca), Achraf Lazaar (Palermo), Hamza Mendyl (Lille), Romain Saïss (Angers).
Viungo, Karim El Ahmadi (Feyenoord), Mounir Obbadi (Lille), Younes Belhanda (Schalke), Abdelaziz Barrada (Marseille), Omar El Kaddouri (Napoli), Fayçal Fajr (Deportivo La Coruna), Youssef Aït Bennasser (Nancy), Nordin Amrabat (Watford), Mehdi Carcela-González (Benfica), Hakim Ziyech (Twente), Mbark Boussoufa (Gent), Walid El Karti (WAC).
Washambuliaji, Khalid Boutaïb (GFC Ajaccio), Oussama Tannane (Saint-Etienne), Badi Aouk (HUSA), Morad Batna (FUS), Yacine Bamou (Nantes), Youssef El Arabi (Granada) Youssef Naciri (Malaga), Abdelghani Mouaoui (IRT), AbderRazak Hamadellah (El Jaish).