Michezo
Himid Mao kuanza mtihani wa majaribio kesho
Kiungo wa klabu ya Azam FC, Himid Mao Kesho Jumanne anatarajiwa kucheza mchezo wake wa kwanza wa majaribio akiwa na kikosi cha akiba cha timu ya Randers FC, inayoshiriki ligi kuu ya nchini Denmark.
Himid Mao aliondoka nchini wiki iliyopita kwenda Denmark kwa ajili ya majaribio na Klabu ya Randers FC inayoshiriki ligi kuu ya Denmark atajifua kesho kwenye mchezo wake wa kwanza wa majaribio.
Taarifa kutoka kwenye mtandao wa klabu hiyo zimesema kuwa kiungo huyo atakuwepo katika mechi hiyo ya kikosi cha akiba cha timu hiyo kabla ya kuamua kumsajili.
“Himid Mao ni mchezaji wetu hivyo nae atakuwa sehemu ya klabu yetu katika mechi ya wachezaji wa akiba dhidi ya AC Horsens “Umeandika mtandao wa klabu ya Randers FC.
By Godfrey Mgallah