Bongo5 Exclusives
Leo Viagra inatimiza miaka 15, ni miongoni mwa dawa zinazouzwa zaidi duniani
Ni miaka 15 tangu Viagra ama Sildenafil citrate, au Revatio iingie sokoni na kwa muda mfupi tu kuwa dawa inayouzika zaidi duniani.
“Viagra was a game-changer,” Dr. Ryan Terlecki, profesa katika hospitali ya Wake Forest Baptist Medical Center huko Winston-Salem, N.C. Marekani ameiambia ABCNEWS.”Ilileta mapinduzi kwenye afya ya mapenzi kwa wanaume na afya yao kwa ujumla.”
Awali Kidonge hicho kidogo cha rangi ya blue kilitengenezwa kutibu tatizo la ‘pulmonary hypertension’ ugonjwa ambao hufanya kifua kibane na mtu kupumua kwa shida. Na sasa wanaume wengi huitumia kuwaongezea nguvu katika mechi zao za kitandani. Tangu miaka 15, Viagra imeshatumika kujaribu kutibu magonjwa kibao na kufanikiwa katika mengi.