Lukamba: Diamond hawawezi kunichukia ananijua vizuri
Kwa mara ya kwanza @lukambaofficial ameweka wazi kilichomuondoa kwa @diamondplatnumz na kuamua kufungua kampuni yake ya @imagixmedia_tz
Akiongea na @el_mando_tz @lukambaofficial ameeleza kuwa watu wanaomzunguka @diamondplatnumz ni wanafiki sana kwani wanajifanya wanamjua @diamondplatnumz zaidi kuliko familia zao.
@lukambaofficial ameongea yote kuhusu maisha aliyokuwa akiishi wakati anafanya kazi na @diamondplatnumz na maisha baada ya kuacha kufanya kazi na @diamondplatnumz
“Watu walio karibu na Diamond walimwambia eti mimi namloga ili niwe nasafiri naye kwenye Ulaya na mataifa mbalimbali, hawakujua kama mimi nasafiri kikazi, Diamond na familia yake hawawezi kunichukia mimi milele maana wananijua vizuri tabia yangu, Diamond ana roho ya kipekee sana” aliongeza Lukamba