Burudani
Mabeste kutoa documentary ya maisha yake,video ya ‘Nishauri’ na wimbo mpya
Rapper Mabeste amesema mwaka huu ameanza kuandaa documentary inayoelezea maisha yake, pamoja video ya wimbo wake ‘Nishauri’itayotoka hivi karibuni pamoja na wimbo mpya.
Akizungumza na Bongo5 leo, Mabeste amesema documentary ya maisha yake itatoka mapema mwezi wa tano baada ya kumaliza,kwakuwa itambidi asafiri sehemu mbalimbali alikofanyia maisha yake.
“Mwaka 2014 umeanza mimi kama mimi nimeanza kushoot documentary inayoelezea maisha yangu kiujumla.Katika muziki nina nyimbo tano mpya ambazo siwezi taja nitaachia ipi,lakini hivi karibuni nitaachia video ya wimbo wangu ‘Nishauri’ pamoja na wimbo mpya,” alisema Mabeste.