Bongo5 ExclusivesHabariSiasa
Mkuu wa Majeshi Mabeyo, Aaga rasmi akiwa Mwanza
Kauli ya Mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama nchini CDF VENANCE MABEYO alipokutana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kuwaaga wana Mwanza na wakazi wa Kanda ya Ziwa baada ya kulitumikia Taifa kwa miongo minne. Mkuu wa Majeshi VENANCE MABEYO alijiunga na jeshi mnamo mwaka 1979 baada ya vita vya Kagera.
“Ninawaaga rasmi kwa sababu ninafikia mwisho wa utumishi wangu Jeshini , Kanda ya Ziwa ndio nyumbani nitarudi nyumbani kupumzika niangalie namna nyingine ya maisha. Nitaendelea kulipenda jeshi hata nikiwa nje ya utumishi wa jeshi,tumekua tukishirikiana katika majukumu mbalimbali yote kuhakikisha taifa letu linabaki salama sisi ni jeshi la wananchi ni sehemu ya wananchi hatuna budi kuwatumikia wananchi”