Burudani
Mwanaume wa Kenya aolewa na Profesa wa Marekani
Mwanaume anayetokea Nakuru, Kenya mwenye makazi yake Marekani, Jumamosi iliyopita aliolewa na mwanaume mwenzake, kwenye sherehe iliyohudhuriwa na marafiki na familia.
Ben Gitau akiwa na mume wake Steve Damelin
Harusi hiyo ilifanyika Ann Arbor, Michigan. Ben Gitau, 33 alifunga ndoa na Mmarekani ambaye ni Profesa wa Hesabu Steve Damelin.
Ndoa hiyo ambayo inaruhusiwa kwenye jimbo la Michigan ilimfanya Gitau awe mke halali wa Professor Damelin. Hatua hiyo imekosolewa vikali kwao Kenya kutokana na mapenzi ya jinsia moja kuwa yanapigwa marufuku.