Ole Gunnar Solskjaer aandika orodha ya majina haya matatu kutua Man United
Manchester United imeandaa orodha ya wachezaji watatu wanaowatarajia kuwasaini dirisha lijalo la usajili ambao ni Ousmane Dembele, Timo Werner na Moussa Dembele.
‘The Red Devils’ imeandaa orodha hiyo ili kuziba nafasi ya nyota wake waliyomuuza Romelu Lukaku huku Alexis Sanchez wakimtoa kwa mkopo.
Manchester United ikimuhitaji, Ousmane Dembele
Meneja wa United, Ole Gunnar Solskjaer sasa amewachagua wacheaji hao watatu akiamini kuwa endapo akipata saini zao basi wanaweza kuipeleka timu hiyo katika ‘level nyingine’.
‘Forward wa klabu ya RB Leipzig Mjerumani, Timo Werner
Kwabahati mbaya sana wachezaji ambao kocha, Ole Gunnar Solskjaer amewaorodhesha watahitaji dau nono ili kuweza kukubali kuangusha saini zao ndani ya Old Trafford hii ni kutokana na ubora waliyokuwanao.
Mshambuliaji wa klabu ya Lyon, Moussa Dembele
Anthony Martial amekuwa nje tangu mwezi Agosti wakati Marcus Rashford na Mason Greenwood wakiwa bado hawajakuwa sawa katika ‘fitness’.
Mashetani hao wekundu wamekuwa wa mwisho miongoni mwa timu ambazo zimeonyesha nia ya kumsaini mchezaji, Martin Odegaard kwa mujibu wa ‘The Sun’.