Quick Rocka atia neno mvutano wa Barakah The Prince na Ben Pol
Msanii wa Bongo Fleva, Quick Rocka amesema wimbo mpya wa Ben Pol ‘Tatu’ aliomshirikisha Darassa kwa upande wake anaona ni mzuri kwani amekuja na kitu kipya chenye ubunifu.
Wiki iliyopita msanii Barakah The Prince kupitia kipindi cha XXL cha Clouds FM alimkosoa Ben vikali kwa kudai wimbo huo ni mbaya kulingana na tension aliyoitengeneza mwanzo.
Quick Rocka amekiambia kipindi cha E Newz cha EATV, kauli ya Barakah The Prince ni kama mtazamo tu wa kila mtu huwezi kumzuia mtu kuongea kama kitu ni kibaya kwanini aseme anapenda wakati hajakipenda.
“Huo ni mtazamo wake mimi naona wimbo ni mzuri, amekuja na idea tofauti. Darassa kachana vizuri, beat Tiddy Hotter kapiga vizuri, it nice song kwangu mimi. Sasa ungemtafuta Barakah akuambie yeye ameona ubaya gani,” amesema Quick.
Msanii huyo ameongeza kuwa kinachotokea kwa Ben Pol sasa hivi maana yake anakua zaidi, changamoto zinapozidi kwenye maisha maana yake unapanda step halafu mambo yanakuwa mazuri.
By Peter Akaro