Burudani

Ripoti: Watu wavamia studio za Tongwe na kumteka Roma na Moni Central Zone

Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule aka Professor Jay, amesema rapper Roma Mkatoliki pamoja na rapper Moni Central Zone wamechukuliwa na kupelekwa kusikojulikana na watu waliozivamia studio za Tongwe Records jana usiku.

Profesa amedai watu hao wamemchukua pia kijana wa kazi, computer ya studio pamoja na TV.

Hii ni taarifa yake:

ROMA MKATOLIKI AMEKAMATWA USIKU HUU… Nimestushwa sana kusikia kuwa kuna watu wamevamia studio za TONGWE RECORDS majira ya saa moja usiku na wamemchukua ROMA @roma2030 , MONI @moni_centrozone na kijana wa Kazi na pia wamechukua COMPUTER ya studio na Screen (Tv) na wameondoka navyo kusikojulikana.. Mpaka sasa hatujui wamewapeleka wapi!!

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents