Burudani
Taylor Swift ampiku Kim Kardashian taji la staa mwenye followers wengi zaidi Instagram
Muimbaji Taylor Swift amefanikiwa kumuondoa Kim Kardashian na kuwa ndiye staa mwenye wafuasi wengi zaidi kwenye mtandao wa Instagram kwa sasa.
Taylor amefikisha zaidi ya followers 45,655,078 na kumuacha Kim aliyesheherekea kufikisha followers milioni 45 wiki iliyopita. Kwa sasa Kim K ana followers 45,571,132.
Kabla ya hapo Taylor alikuwa katika nafasi ya tatu huku juu yake wakiwepo Beyonce na Kim K. Beyonce kwa sasa ana followers 45,080,613.