Michezo

Timu hizi zafuzu kwa mara ya kwanza kombe la Shirikisho Barani Afrika

 

Kuna jumla ya timu nane zimefanikiwa kufuzu kwa mara ya kwanza kwenye hatua ya makundi ya michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

Kutoka Ghana kuna timu ya Aduana, upande wa Congo, CARA, Williamsville ya Ivory Cost, UD Songo ya Mozambique, El Masry ya nchini Misri, huko Moroccan ni RS Berkane wakati kwa upande wa Afrika Mashariki ni Gor Mahia ya Kenya na Rayon Sports ya Rwanda hizo ndizo timu ngeni zilizofanikiwa kuingia hatua hiyo kwa mara ya kwanza.

Kwenye timu ambazo zimeingia hatua hiyo ni pamoja na miamba ya soka ya zamani ya Afrika, AS Vita (DR Congo), Raja Club Athletic (Morocco), ASEC Mimosas (Ivory Coste) na Enyimba (Nigeria). CARA, zikiwa zinajumuisha timu 16 bora.

Lakini pia kwa upande wa Malia ipo Djoliba, USM Alger (Algeria), Young Africans (Tanzania) na El Hilal (Sudan).

Droo ya hatua hiyo ya makundi inatarajiwa kufanyika leo siku ya Ijumaa Aprili 21 majira ya alasiri makao makuu ya CAF, Cairo, Misri.

Hizi ndizo timu zote 16 zitakazo shiriki hatua hiyo ya makundi ya mashindano ya kombe la Shirikisho Afrika.

AS Vita (DR Congo), USM Alger (Algeria), El Masry (Egypt), Raja Club Athletic (Morocco), CARA (Congo), El Hilal (Sudan), Gor Mahia (Kenya), UD Songo (Mozambique), Enyimba (Nigeria), Aduana (Ghana), Young Africans (Tanzania), RS Berkane (Morocco), Williamsville (cote d’Ivoire), Djoliba (Mali), Rayon Sports (Rwanda)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents