BurudaniDiamond Platnumz
Wimbo wa Diamond wamtoa Nisha machozi
Wimbo wa msanii Diamond Platnumz ‘Sikomi’ umeukonga moyo wa muigizaji Nisha kiasi kwa mrembo huyo kububujikwa na mazozi.
Wimbo huo ambao maudhui yake unazungumzia mapenzi kwa mtu ambaye ametendwa, unasikika katika video ambayo ameiposti Nisha katika ukurasa wake wa Instagram ambapo anaonekana akilia.
Soma Pia; Snura afunguka kukwapua mpenzi wa Nisha
Hivi karibuni kumekuwa na stori kuwa aliyekuwa mpenzi wa Nisha kwa sasa anatoka kimapenzi na msanii Snura, hata hivyo muimbaji huyo amekuwa akikanusha hilo kwa kueleza wapo pamoja kikazi tu na si vinginevyo.