Michezo

Yaelezwa mwili wa mtu aliyekufa wakutwa kwenye nyumba ya kiungo huyu wa Arsenal

Yaelezwa mwili wa mtu aliyekufa wakutwa kwenye nyumba ya kiungo huyu wa Arsenal

Mwili wa mtu umepatikana nyumbani kwa kiungo wa kati wa Arsenal Mohamed Elneny nchini Misri.

Babake Elneny, Nasser aliupata mwili huo wakati alipotembelea nyumba hiyo mjini Mahalla al-Kubra , ambayo iko takriban kilomita 100 kaskazini mwa Cairo.

Kwa mujibu wa BBC. Kisa hicho kiliripotiwa kwa polisi, ambaye wanasema mtu huyo alikuwa akijaribu kuiba nyaya za umeme.

Inaaminika kwamba alichomwa na umeme wakati wa wizi huo. Nyumba hiyo ni mali mpya ambayo ilitolewa na familia ya Elneny kutumika kama ofisi.

Elneny ambaye amerudi Arsenal baada ya kuichezea Misri katika kombe la mataifa ya Afcon , aliambiwa kuhusu kisa hicho kupitia simu.

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents