Burudani
Young Dee: Niliwahi kujutia umaarufu wangu
Rapper Young Dee amesema amewahi kujutia kuwa mtu maarufu kutokana na kukosa pesa zinazolingana na jina lake.
Akiongea na E-News ya EATV, Young Dee alisema,” Tokea nimekuwa Young Dar es Salaam, sijawahi kujuta lakini nilijuta nilivyokuwa Young Dee mwanzo wakati naanza. Si unajua ndo nilikuwa nimetoa ngoma yangu ya kwanza halafu bado sina kitu alafu inabidi upande daladala halafu unakutana na madenti wamekaa siti ya nyuma wanaanza ‘Young Dee’ wanazingua kweli yaani.”
“Ile ilikuwa inanitesa sana maana nilikuwa naona nashindwa kuwa huru na maisha yangu yaani kuwa mtu wa kawaida tu nikapanda daladala nikakaa poa tu. Lakini ilikuwa ngumu hiyo hali ilikuwa inanitesa sana kipindi cha nyuma.”