Michezo
Zidane aweka rekodi mpya klabu bingwa Ulaya
Kocha wa klabu ya Real Madrid, Zinedine Zidane ameweka rekodi ya kuwa kocha wa kwanza kulitetea kombe la Ligi ya mabingwa barani Ulaya.
Madrid imeshinda ubingwa wa Ulaya kwa ngazi ya vilabu jana usiku ilipovaana na Juventus kwa mara ya pili mfululizo.
Msimu uliopita 2015/16 Real Madrid walishinda kombe hilo dhidi ya Atletico Madrid, na jana wamefanya hivyo kwa kuichapa Klabu ya juventus goli 4-1.
Zidane anakuwa Kocha wa kwanza kuwahi kutokea kulitetea kombe hilo lenye ushindani zaidi barani Ulaya.