Burudani
Baby J aomba wasanii kujitangaza Ziff
Mwanamuziki toka Zanzibar Jamila Abdallah maarufu kama Baby J (Wa katikati) akiwa na rafiki zake Janert Masanja na Valentina Mvumvu, akiongea na Bongo5 alisema wasanii wasisubiri sana kualikwa kwani hata wao wananafasi ya kuomba ilikuweza kujitangaza kimataifa zaidi.
Alisema mtu kujipendekeza kwa manufaa yake si kibaya sana kwani kukosa tamasha hilo ni sawa na kupoteza kitu cha muhimu katika sanaa yake.
Pia Baby J, alisema hivi sasa anatarajia kuja na wimbo wake mpya inayokuja kwa jina la Furaha yangu.
Pia amesema kwa sasa anatembea na wacheza shoo wake popote pale kwaajili ya kumsaidia katika kunengua na kubwabwajua katika jukwaa.