Michezo
Lionel Messi ndiye mchezaji wa soka mwenye thamani kubwa zaidi duniani
Mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi ndiye mchezaji wa soka mwenye thamani kubwa zaidi duniani.
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na CIES Football Observatory, thamani yake ni mara mbili ya Cristiano Ronaldo. Utafiti huo umebaini kuwa mchezaji huyo wa timu ya taifa Argentina ana thamani ya £161.5m huku Ronald akikamata nafasi ya 2 akiwa na £85.2m na mchezaji wa Liverpool Luis Suarez akiwa na £79.4m.
Mchezaji wa Chelsea, Eden Hazard amekamata nafasi ya nne akiwa na £61.2m na kufuatiwa na Neymar akiwa na £50.6m. Naye Gareth Bale amekamata nafasi ya saba akiwa na £50.9m.