Burudani

Pascal Kassin wa BSS: Nimepona ila nguvu za kiume bado, mke wangu wamevumilia ila … (Video)

Mshindi wa BSS mwaka 2009, Pascal Kassian amefunguka mazito ikiwa ni mwaka mmoja toka arudi Dar Es Salaam akitokea India kwaajili ya matibabu baada ya kupata ajali ya gari .

Gharama hiyo ya matibabu iligharamiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda baada ya kukaa muda mrefu bila msaada.

Akizungumza na BongoTV wiki hii, Pascal amesema anamshukuru Mungu amepona kabisa ingawa nguvu zake za kiume zimeshindwa kurudi hivyo anashindwa kumpatia haki mke wake wa ndoa.

Amesema hali hiyo amejaribu kujitibu toka mwaka jana lakini bado mambo hayajakaa vizuri huku akimwagia sifa mke wake kwa kumvumilia katika kipindi hicho chote.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents