Mitindo

Nguo ya rangi nyeusi ni kali na inavutia sana

Hellow! Karibu katika ulimwengu wa mitindo kutoka hapa Bongo5, leo nataka tuzungumzie vazi la nguo nyeusi jinsi linalovyoweza kukuokoa usihaibike kwenye shughuli mbalimbali. Mara nyingi tumekuwa tukitamani kubadiri rangi za nguo zetu, ziwe kwa wanaume ama wanawake.

Ni vizuri kuepuka kuvaa nguo zenye rangi angavu hasa kwenye mitoko yetu muhimu na tuipendayo, Kwanikutumia rangi nyingi katika nguo moja unaweza ukakosea jambo dogo sana katika uvaaji na likaharibu muonekana wako mzima na ukatamani kupotea eneo hilo kutokana na aibu utakayoipata hasa pale watu na wabunifu wa mavazi watakapo kutolea macho.

Kwanini Nyeusi:- Hii ni kutokana kwamba rangi nyeusi inaendana na tukio lolote kama unaweza ku-note, katika kabati lako lazima kuna nguo nyeusi. Mara nyingi rangi ya nguo hiyo huwa kama ni mokozi wetu hasa kwa wanaoogopa kukosea kuchanganya rangi katika nguo moja.

Hata wanaume wengi wamekuwa na idadi kubwa ya nguo nyeusi, ndio maana unakuta mwanaume anasuruali tatu nyeusi na mashati mengi hapo ndo unajua kuwa rangi hiyo ni muhimu kuwa nayo katika makabati yetu ya nguo.

Nakumbuka niliwahi kusemea si vibaya kujaribu rangi ila sio kila rangi ya kuijaribu.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents