Habari

Benki ya Exim yaandaa iftar kwa wadau wake wote

 Benki ya Exim imeandaafutari ya pamoja kwa wateja wake katika hafla iliyofanyikakatika hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam mnamo tarehe15 mwezi Machi 2024.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Jaffari Matundu, akizungumza na wadau (hawapo pichani) katika hafla ya Iftar iliyoandaliwa na benki hiyo kwa lengo la kuimarisha uhusiano kati ya benki na wadau wake wakiwemo wateja na jamii katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani katika tukio lililofanyika tarehe 15 Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam
IFTAR: Wadau mbalimbali na wawakilishi wa Benki ya Exim wakifurahia Iftar iliyoandaliwa na benki hiyo kwa lengo la kuwaleta pamoja katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani kuashiria furaha, umoja, na upendo katika tukio lililofanyika tarehe 15 Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

 

Mgeni Rasmi katika tukio hili alikuwa Sheikh Mkuu waMkoa Dar es Salaam, Sheikh Walid Alhad Omar, akiwakilisha waumini wa dini ya Kiislam ambao wapokwenye mfungo katika mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani.

 

Akizungumza katika hafla hiyo, Sheikh mkuu wa mkoa waDar es salaam, Sheikh Walid Alhad Omar, aliipongeza Benkiya Exim kwa juhudi zake katika kukuza maendeleo yakijamii na kueleza shukrani zake kwa mchango wa benkihiyo kwa jamii. Alisema, “Benki ya Exim inaonyeshadhamira ya kweli katika kutumikia wateja wake na jamiikwa ujumla, lengo kuu la Ramadhani ni kuleta watu pamoja, na usiku huu, benki ya Exim imehakikisha kuendeleza lengohilo kwa vitendo”.

 

Bwana Jaffari Matundu, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki yaExim, aliwakaribisha wadau wote katika Iftar hiyo hukuakitambua mahusiano mazuri ya tija yaliopo baina ya Benkiya Exim na wateja wake na umuhimu wa kuyaendeleza kwaajli ya ustawi na maendeleo ya jamii.

 

“Wateja wetu ni zaidi ya wateja tu, ni sehemu muhimu ya familia yetu. Tunaona kila mmoja wenu kama mshirika namwenzetu katika safari yetu ya mafanikio”, alisisitiza JaffariMatundu.

 

Pia, Mkurugenzi huyo alizungumzia hatua na maboreshombalimbali ambayo yamefanywa na benki ya Exim ilikuendana na mabadiliko katika sekta mbalimbali ikiwemomaendeleo ya teknolojia ya kidijitali na kusogeza hudumakwa wateja.

 

Jaffari alifafanua kuwa, “tumefanya maboresho makubwa katika mfumo wetu wa Benki ili kuendelea kuhudumia wateja wetu vizuri zaidi kwa kutoa huduma zinazoendana na mabadiliko ya kidigitali”.

 

“Vile vile tumeendelea kuongeza idadi ya Mawakala wetu (maarufu kama Exim Wakala) ili kuleta huduma zetu karibuna wateja wetu popote walipo”, alimalizia Afisa MtendajiMkuu huyo.

 

Exim Bank pia imeboresha huduma za kidijitali kwa watejawake ambapo wanaweza kupata huduma za kibenki popotepale walipo ndani na nje ya Tanzania. Hii ni kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma za kibenki kwa watejawao na maendeleo ya teknolojia yanayoendelea kutokeaduniani.

 

 

IFTAR: Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Walid Alhad Omar, akitoa pongezi kwa Benki ya Exim kwa kuandaa Iftar akielezea namna ambavyo imewaleta pamoja waumini wa dini ya kiislam kama ishara ya upendo, umoja na heshima kwa wadau wote katika hafla hiyo iliyofanyika tarehe 15 Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
IFTAR: Sheikh Mkuu wa Dar es Salaam Sheikh Walid Alhad Omar (katikati) na Afisa Mtendaji Mkuu wa Exim Bank, Jaffari Matundu (watatu kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na wadau wa benki hiyo wakati wa hafla ya Iftar iliyoandaliwa na benki hiyo kwa lengo la kuwakutanisha wateja wake pamoja katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani iliyofanyika tarehe 15 meezi Machi 2024 katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents