Davido asaini mkataba mwingine na RCA Records
Bosi wa lebo ya DMW, Davido amesaini mkataba mwingine na label ya RCA Records.
RCA Records inawasimamia wasanii wakubwa wakiwemo ASAP Ferg, ASAP Rocky, Alicia Keys, Aretha Franklin, Zayn Malik, Usher, T-Pain, Shakira, Justin Timberlake, Pink na wasanii wengine wengi.
Mmoja kati ya watu wa karibu wa Davido, Efe Ogbeni kupitia akaunti yake ya Instagram ameandika, “Welcome to #RCA @rcarecords @davidoofficial ” chairman #peteredge we start the GRIND #afrofusion is here,” and “am all into TEAM WORK @tunji (#brysontiller ) chairman RCA #peteredge Global superstar @davidoofficial his manager.. Brains @kamalajiboye.”
Hata hivyo bado Davido anaendelea na mkataba wake na kampuni ya Sony Music Global aliosaini mapema mwezi January mwaka huu utakaompa nafasi ya kuwa msanii ambaye muziki wake utasambaa duniani kote.