Michezo
Hector Bellerin atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa wiki 3 hadi 4
Mchezaji wa klabu ya Arsenal, Hector Bellerin atakaa nje ya uwanja kwa muda wa wiki 3 hadi 4 kufuatia kusumbuliwa na maumivu ya kifundo cha mguu aliyoyapata kwenye mechi dhidi ya Spurs jumapili ya wiki iliyo pita.
Hector ambaye alikuwa katika timu ya Taifa ya Hispania chini ya miaka 21, alilazimika kujitoa ili kufanyiwa vipimo na timu ya madaktari wa Arsenal.
Hivyo Bellerin atakosa mechi zote za mwezi Novemba zikiwemo zile dhidi ya Man United pamoja na Psg katika klabu bingwa Ulaya.