Burudani
Julio wa BBA Stargame aachia single ya kwanza ‘Cheers’
Hatimaye aliyekuwa mwakilishi wa Tanzania katika shindano la Big Brother Africa mwaka jana, Julio, ameachia single yake mpya.
“Track inaitwa CHEERS…..ka produce Frankboi ambaye kwa sasa hayupo mjini yupo Marekani,” amesema Julio kwenye maelezo yake.
“Nimeingiza sauti na mixing kwa Lucci Da Don. Tayari nina track kumi ambazo zitakuwa kwenye double CD album ya 600 music mimi na mshkaji wangu mjengoni anaitwa Seydou Soumare. So hii dedicated to Tanzania…nimeingia kwenye game na track kali kibao zinakuja,na ntafanya collabo na wasaniii wa Bongo flavour ambao wanataka kutoka kiiinternational…maana mi na rap Kiingereza for international market.”
Download it Here