Michezo

Klabu ya Fenerbahce ya wataoa hofu mashabiki wa Van Persie

Klabu ya Fenerbahce ya nchini Uturuki, imetoa taarifa kwa mashabiki wake baada ya jeraha la jicho alilopata mshambuliaji wa zamani wa Arsenal na Manchester United Robin van Persie.

3a20129900000578-0-image-a-3_1478462672728

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 33, alifunga bao la kuongoza katika mchezo wa ligi uliochezwa jana dhidi ya Akhisar ambao walikubali kufungwa mabao matatu kwa moja.

3a20194400000578-0-image-a-16_1478464082242

3a20193c00000578-0-image-a-14_1478464061685

Katika dakika ya 37 Van Parsie alishindwa kuendelea na mchezo baada ya kupata jeraha la jicho na kulazimika kutolewa nje ya uwanja kwa usaidizi wa watu wa huduma ya kwanza, baada ya kugongana na mchezji wa timu pinzani.

3a20194000000578-0-image-a-15_1478464079007

Baada ya mchezo kumalizika uongozi wa Fenerbahce ulitoa taarifa njema kwa mashabiki ambazo zilieleza Van Parsie anaendelea vizuri.

“Alipatwa na tatizo la jicho lakini kwa uchunguzi wa awali imeonekana sio kubwa sana,” ilieleza taarifa ilitotolewa na daktari Burak Kunduracıogl.

“Tumejiridhisha jeraha lake halitomuweka nje kwa muda mrefu, lakini kwa siku kadhaa atakua katika uangalizi wa kimatibabu.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents