Burudani
P-Square waahidi kupiga show kali leo Leaders Club, Dar
Waswahili wanasema asiye na mwana aeleke jiwe leo, kwakuwa mapacha wanaopendwa zaidi Afrika, P-Square wataangusha show ya mwaka kwenye viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam.
Wakiongea na waandishi wa habari jana, mapacha hao wamesema Tanzania leo itashuhudia show kali kutoka kwao hasa kwakuwa tangu waje mara ya mwisho, miaka mitano iliyopita, wameshaachia hits kibao ambazo hawajaziimba live nchini,. Hits hizo ni pamoja na Chop My Money, Alingo na Personally.
P-Square watasindikizwa na Lady Jaydee, Joh Makini, Profesa J na Ben Pol.