Burudani
Picha: Ex wa Luteni Karama, Isabela aangukia kwa mzungu huyu
Aliyekuwa mpenzi wa zamani wa msanii wa Kundi la Gangwe Mob Luteni Karama, Isabela, ameamua kumuweka wazi mpenzi wake mzungu ikiwa ni miezi michache toka mpenzi wake huyo wa zamani afunge ndoa na rafiki yake wa karibu.
Isabela akiwa na mpenzi wake
Akiongea na Bongo5 Jumatano hii, Isabela adai kwa sasa amempata mtu sahihi ambaye amemsahaulisha yaliyotokea nyuma.
“Huyo ndio mpenzi wangu kwa sasa, kwa hiyo nipo sehemu salama kabisa,” alisema Isabela.
Hapo awali, muimbaji huyo alidai kuumizwa na kitendo cha aliyekuwa mpenzi wake huyo kufunga ndoa na rafiki yake wa karibu.