Uncategorized
Swahiba wa ‘El Chapo’ atiwa nguvuni nchini Mexico
Swahiba wa aliyekuwa mfanyabiashara maarufu wa dawa za kulevya duniani na Kiongozi wa kundi la Sinaloa Cartel, Joaquin Guzman maarufu kwa jina la ‘El Chapo’ amekamatwa jana nchini Mexico.
Mamlaka nchini Mexico zimesema kuwa Damaso Lopez rafiki yake na ‘El Chapo’ alikamatwa katika mji wa Mexico City kwa tuhuma za kusafirisha tani za Madawa ya kulevya kwenda nchini Marekani.
Tangia kukamatwa kwa aliyekuwa kiongozi kundi hilo Joaquin Guzman ‘El Chapo’, viongozi wa juu wa kundi maarufu linalojihusisha na biashara ya madawa ya kulevya la Sinaloa Cartel, limekuwa likisambaratika kila kukicha kwa kung’ang’ania madaraka hali iliyopelekea kuibuka kwa uhalifu katika maeneo ya Sinaloa,nchini Mexico.
By Godfrey Mgallah