Videos

Vanessa Mdee awakusanya Osse, Pedaiah, Shadee na Chunie kwenye video ya Closer

Baada ya kusubiri kwa muda mrefu hatimaye video ya wimbo wa kwanza wa Vanessa Mdee, Closer, imetoka. Video hiyo imetengenezwa na kampuni ya Ogopa Videos ya nchini Kenya. Katika video hiyo kali, Vanessa anaonekana akiimba kwenye ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es Salaam pamoja na Velisa huku camera za Ogopa zikichukua mandhari mazuri ya eneo hilo na kutengeneza picha inayovutia na kukufanya uhisi unaona mandhari ya Miami Beach!!

http://youtu.be/yKMT4cwvy-8

Kwenye video hiyo, Vanessa amewatumia warembo Shadee na Chunie pamoja na mamodel Osse Sinare na Pedaiah Swank John. Enjoy.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents