Burudani
Wimbo wa Diamond na Donald wa SA unaitwa Wangu na utatoka Ijumaa ijayo
Wimbo unaosubiriwa kwa hamu kubwa kati ya Diamond Platnumz na msanii wa R&B wa nchini Afrika Kusini, Donald unaitwa Wangu.
Wimbo huo uliorekodiwa kwenye studio za Universal Music nchini Afrika Kusini na video yake kufanyika nchini humo utatoka Ijumaa, July 17.
Video ya wimbo huo pia itatoka siku hiyo hiyo.
“ANNOUNCEMENT: #Wangu officially drops next week friday the 17th. The video drops on the same day #DonaldAndDiamondCollabo,” ameandika Donald kwenye Instagram.