Burudani
French Montana aahidi kuachia albamu yake mpya mwezi Julai
Baada ya muda mrefu kupita bila ya kuwa na albamu sokoni, hatimaye rapper French Montana ametangaza ujio wa albamu yake mpya.
Albamu hiyo ambayo imepewa jina la Jungle Rules, inatarajiwa kutoka Julai 14 ya mwaka huu. Rapper huyo alisema hayo wakati akitumbuiza katika jukwaa la BET wikiendi iliyopita.
Mara ya mwisho Montana aliachia albamu yake ya Excuse My French, Mei 2013.