Mwanamuziki Karapina amesema kwa sasa anatarajia kubadili mfumo wa maisha yake ya kimuziki, na kuufanya kama kazi kwaajili ya kumuandalia maisha mazuri mwanaye Hindu.
Alisema mtoto huyu aliyezaa na mkewe ambaye walifunga ndoa muda mrefu, amempa jina la mama yake Bi Hindu kama vile kumuezi. Pia amesema angefurahi sana kama mwanaye atakuja kuwa kiongozi wa kundi lolote, hata kama akiwa mwanamuziki.