Tragedy
P-Diddy hatunaye tena.
Habari za kusikitisha zimetufikia kwamba Perfect Kagisa aka P-Diddy, (picha ya chini) ambaye alikuwa mmoja kati ya wakurugenzi wa bendi ya Diamond Musica amefariki dunia leo mchana baada ya kudondoka ghafla mitaa ya Lumumba akiwa katika harakati za kufanya shughuli zake.
Perfect pia alikuwa maarufu kama mchumba wa miaka mingi wa Maimartha Jesse mtangazaji maarufu TBC1.
Tunaiombea roho ya mrehemu ilale mahali pema peponi na Mungu awape nguvu ndugu, jamaa na marafiki wa Marehemu.