Michezo
Debuchy ampa wasiwasi Arsene Wenger
Mchezaji wa klabu ya Arsenal Mathieu Debuchy kuna wasiwasi kwamba jeraha alilolipata siku ya Jumapili ni baya, kocha Arsene Wenger amesema.
Debuchy, 31, ambaye alicheza kwa mara ya kwanza tangu Novemba 2015 mechi ya Ligi ya Premia dhidi ya Bournemouth ambayo walishinda 3-1 lakini akaumia misuli ya paja na kulazimika kuondoka uwanjani baada ya dakika 16.
“Itanibidini kuzungumza na matabibu, lakini unaweza tu kujua hali halisi baada ya saa 48,” alisema Wenger.
“Unahitajika kuacha damu itoke kisha baadaye tuwe na uchunguzi wa MRI baada ya saa 48 kubaini ubaya wa jeraha.”
Magoli ya Arsenal katika mechi hiyo yalifungwa na Alexis Sanchez mabao mawili na moja la Theo Walcott.